Quantcast
Channel: D'JARO ARUNGU
Viewing all 2632 articles
Browse latest View live

Stara Thomas aandika wimbo kuhusu Facebook.

$
0
0
Hii inatokana na jinsi ilivyo na wafuasi wengi ‘active member takribani bilioni 1.9’, na hivyo mengi yanazungumziwa huko na bahati mbaya mengine huwekwa bila kuthibishwa.
Kwa kuzingatia hayo, mwimbaji mkongwe wa Tanzania, Stara Thomas ameamua kukaa chini na kuandika wimbo kuhusu mtandao huo wa kijamii ‘Facebook’.
Mwimbaji huyo wa ‘Wasiwasi wa Mapenzi’ ameweka wazi mpango huo wakati akizungumza katika kipindi cha Hatua Tatu cha 100. 5 Times Fm, baada ya msikilizaji mmoja kutaka kufahamu kama kweli amehama VOA band ya Linex.
“Nadhani mara nyingi mtu anapokuwa anaongea jambo…tumekuwa na tatizo la Facebook ndani ya ubongo. Facebook inadaka halafu inajibu hapo hapo.” Amesema Stara Thomas.
“Na kuna wimbo naandika kuhusu Facebook, really I’m telling you. Na Times Fm itakuwa ya kwanza kuucheza.” Ameongeza Stara, kisha akalijibu swali la msikilizaji.
“Kwenye VOA band, sio kana kwamba ni bendi ambayo tunapiga kila siku. Yeye ana project zake, na mimi naproject zangu lakini pale tunapotaka kufanya kwa pamoja tunafanya kwa pamoja, lakini sio kwamba ni bendi tunayopiga kila siku.”
Stara Thomas alisisitiza kuwa bado hajatoka VOA band.

KESI YA MAUAJI YA MWANDISHI WA HABARI MWANGOSI YANGURUMA.

$
0
0

Kesi ya mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten,
marehemu Daudi Mwangosi inayomkabili aliyekuwa askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mwenye namba G. 2573 Pacificus Cleophase jana ilianza kusikilizwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Iringa.

Wakati kesi hiyo ikisikilizwa, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa mmoja kati ya 11 wanaokabiliwa na kesi ya mauaji ya kukusudia ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi, Longishu Losingo (29) amelalamika kuwa wanalishwa mchuzi wa maharage gerezani.

Kesi hiyo ya Mwangosi inasikilizwa na Jaji Mfawidhi, Mary Shangali.

Wakili wa Serikali, Adolf Maganda alidai kuwa mtuhumiwa Cleophase ambaye alikuwa askari polisi mkoani Iringa alifanya mauaji hayo Septemba 2 mwaka 2012 katika eneo la Nyololo, wilayani Mufindi.

“Mshtakiwa alitenda kosa hilo wakati alipokuwa akiwaamuru wafuasi wa Chadema kuondoka katika eneo la tukio walipopanga kufanyia mkutano,” alidai.

Maganda alidai kuwa katika tukio hilo, mtuhumiwa alifyatua risasi na kumpiga marehemu.

Wakili huyo alidai kuwa wafuasi wa Chadema walifika katika eneo hilo kwa ajili ya kuhudhuria mkutano ambao katibu mkuu wa chama hicho alikuwa anatarajia kuhutubia.

Alisema mkutano huo ulikuwa ufanyike licha ya polisi kuwaandikia Chadema ikiwataka wauahirishe ili kupisha zoezi la sensa.

Aliendelea kuieleza mahakama kuwa baada ya kuzuiwa kufanya mkutano, wafuasi wa chama hicho walianza kurusha mawe na kuwaumiza baadhi ya askari polisi, hatua iliyowalazimisha kuwatawanya kwa mabomu ya machozi na kwamba hatua hiyo ilikuja baada ya kuwasihi kutokufanya mkutano huo.

Maganda alidai kuwa mshtakiwa akiwa na bunduki alikwenda katika eneo la tukio alilokuwa marehemu na kufyatua risasi na kumpiga marehemu ambaye alikufa papohapo. Alidai kuwa taarifa ya daktari inaonyesha kuwa kifo cha Mwangosi kilisababishwa na kupatwa na majeraha yaliyotokana na mlipuko mkali.
Credits:Mwananchi

AMUUA MWENZAKE WAKIGOMBEA SIGARA.

$
0
0

Uvutaji wa sigara umeleta maafa, baada ya mtu mmoja kukatwa mkono na kuuawa na mwenzake wakati wakigombea sigara.


Katika tukio hilo lililotokea Korogwe, Jumapili iliyopita, Februari 2, mnamo saa nne asubuhi, Idi Mkono, mwenye umri wa miaka 30 alimkata mkono Ramadhani Gudelo (35) na kumuua baada ya kutokea ugomvi uliohusu sigara.

Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Constantine Massawe alisema kuwa Polisi Tanga wako katika msako mkali wa kumtia nguvuni Iddi Mkono (30) kwa tuhuma za mauaji.

Kamanda Massawe ameitaka jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi, badala yake wafuate taratibu na sheria zilizopo.

Wakati huo huo, watu wawili wanashikiliwa na polisi, mkoani hapa kwa tuhuma za kukamatwa na lita 147 za pombe haramu ya gongo maeneo ya Handeni, mkoani Tanga.

Kamanda Massawe alisema kuwa tukio hilo la kukamatwa kwa watuhumiwa hao lilitokea Februari 2 mwaka huu saa 5:30 asubuhi.

Massawe aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Hussen Muhadu (48), pamoja na Ramadhani Ugarawe (40), wote wakazi wa Chanika Handeni.

Alisema jeshi hilo linaendelea na uchunguzi ili watuhumiwa waweze kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayowakabili.

Aidha Kamanda Massawe aliwaonya wananchi kuchukua tahadhari na matendo ya uhalifu wa aina yoyote ambao unaweza kusababisha kuvunja sheria, huku akionya kuwa kwa yeyote atakayekiuka sheria zilizowekwa atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa. 

NIMEKUTA PICHA ZA UTUPU ZA GIRLFRIEND WANGU KWENYE SIMU YAKE..USHAURI PLEASE.

$
0
0

Jamani Wapendwa Valentines imenikalia Pabaya leo yaani, My girl kaja kulala kwangu ili leo tusherekee
wote hii siku kuna mahali tunaenda out of Town, ila sasa asubuhi ya leo wakati tunajiandaa nikachukua simu yake nikawa nampiga picha alivyopendeza baada ya kuvaaa sasa katika kuziangalia zile picha nikakutana na picha zingine za utupu alizopiga like one week ago, Sasa najiuliza hizo picha alipiga kwa ajili ya nani je alimtumia mtu maana kama ni mimi hakunitumia, nimemuuliza anasema alijipiga kujifurahisha, yaani hapa niko nae ila kama simwamini tena jamani naombeni ushauri.

KESI YA KIFO CHA KANUMBA, LULU AKESHA AKIOMBA.

$
0
0
STAA wa Filamu ya Foolish Age, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema hivi sasa anakesha akiomba ili mambo yaende vizuri katika kesi inayomkabili ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba.


Lulu amemwambia paparazi wetu kuwa alishaanza kuyasahau matatizo hayo lakini hataweza kupingana na amri ya mahakama iliyopanga kuanza kusikiliza kesi hiyo kuanzia Februari 17, mwaka huu katika Mahakama Kuu ya Tanzania jijini Dar.

“Lazima kesi iendelee na sheria ichukue mkondo wake, pamoja na kwamba nimekaa uraiani kwa kipindi kirefu na kuanza kusahau mambo hayo,” alisema Lulu.

Alipoulizwa anachokitegemea katika kesi hiyo, msanii huyo alidai kwamba hana cha kukitegemea zaidi  ya kukesha akimuomba Mungu.

“Nakesha nikiomba, namwamini Mungu atanisaidia kama alivyosikia kilio changu cha kuomba dhamana,”aliongeza.

Msanii huyo anakabiliwa na kesi ya kumuua bila ya kukusudia aliyepata kuwa msanii nguli katika tasnia ya filamu za Kibongo, Kanumba Aprili 7, mwaka 2012.

Aidha, baada ya kuachana na Lulu, Ijumaa lilizungumza na mama mzazi wa Kanumba, Flora Mtegoa juu ya kutajwa kwa kesi hiyo na mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo; 
Ijumaa: Unajisikiaje kuona Lulu akipandishwa kizimbani tena?

Mama Kanumba: Mmmh! Kwa kweli najisikia vibaya sana jamani.
Ijumaa: Unajisikia vibaya  kwa kuwa Lulu anapandishwa kizimbani au...?
Mama Kanumba: Pamoja na hilo lakini kesi hii inanikumbusha machungu ya mwanangu, naona mambo ndiyo yamefufuka upya wakati nilishaanza kuyasahau.

Ijumaa: Unasemaje kuhusu kushtakiwa kwa Lulu?
Mama Kanumba: Binafsi sijamshitaki Lulu ni serikali ndiyo iliyofanya hivyo, tuache sheria ichukue mkondo wake.
Credits:Global Publishers 

MC PILIPILI LEO NDANI YA BNN HALL-UCHUMI QUALITY CENTRE.

$
0
0

MC na MCHEKESHAJI Maarufu leo tarehe
14 februari usiku kuanzia saa 1 mpaka liamba
atakuwa na Bonge moja la show pale Uchumi
Nyerere Road katika Ukumi wa Kisasa 
kabisa ya BNN AMBAPO ATASHIRIKIANA 
na ATOMY Sifa Kutoka Nairobi Kenya.


Kiingilio ni sh laki 1 kwa wawili na sh elf 60 kwa mtu 1 ila hiyo bei 
imejumuisha Vinyaji na Vyakula Bure.Hivyo Ukizama tu ndani kwa hiyo kiingilio
kila kitu ni Bure.

Hivyo Wadau wote Tukutane Hapo katika siku hii maalum ya wapendanao.

FUNDI SAMWELI ATHIBITISHA KUACHANA NA MKEWE MWANAMUZIKI SARAHA.

$
0
0

Producer wa wimbo mpya wa Ben Pol, ‘Unanichora’, Fundi Samwel ambaye ni raia wa Sweden, amethibitisha kuachana na mke wake, Saraha.


Mtayarishaji huyo amesema sababu kubwa ya kuachana ni ubusy waliokuwa nao uliosababishwa na muziki na hivyo kuwafanya wasiwe karibu kwa kipindi kirefu.

“Mimi na Saraha tuliachana, kilikuwa kitu kibaya kwangu na kwake pia ndio maana nilikuwa kimya kidogo mwaka huu sababu unajua moyo ulivunjika sana na mood lazima ipotee,” Fundi Samwel amemuambia Sam Misago kwenye kipindi cha Power Jams cha East Africa Radio.

“Unajua kukaa na kufanya muziki lazima utumie muda sana na unatumia akili sana, na hata yeye alifanya kazi nzuri hapa, alikuwa busy sana, namimi nilikuwa busy ya studio. Unajua anakuta foleni kila siku halafu wewe unapiga kazi kama masaa 15 hivi and then unachoka sasa huwezo kuongea vizuri. Hata Saraha alichoka, unajua tulishindwa kuongea vizuri na kitu kiliendelea. And then tulipofika Sweden, unajua upendo uliisha tu, uliisha kabisa,” aliongeza.

Samwel ambaye tayari amerejea kwao nchini Sweden amesema yupo Tanzania kwa wiki mbili kutengeneza nyimbo kadhaa. 

SKENDO ZA ROSE MUHANDO MAPYA YAIBUKA.

$
0
0

JAMBO limezua jambo! Siku chache baada ya staa wa Injili Bongo, Rose Muhando kudaiwa kutiwa mbaroni kwa utapeli wa shilingi milioni 6, nyuma ya skendo hiyo, mapya yameibuka.


Habari hiyo iliruka hewani kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti tumbo moja la hili, Ijumaa Wikienda la Februari 10 hadi 16, mwaka huu ikiwa na kichwa; ROSE MUHANDO MBARONI.

Kwa mujibu wa Katibu wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, Stella Joel, mara kadhaa Rose alishaingia kwenye skendo nyingi kutokana na jamaa aliyetajwa kwa jina la Nathan Wami.

Alisema katika albamu ya Rose ya kwanza kabisa iitwayo, Jipange Sawasawa alijikuta akiingia kwenye balaa la kubambikiwa msala wa kudaiwa kukutwa na madawa ya kulevya ambapo katika mazingira yeye utata, staa huyo alijikuta akiziachia shilingi milioni 30 bila kujijua kwa baadhi ya polisi wa Dodoma. Hiyo inadaiwa ilikuwa ‘karibisha mgeni’

Stela alifafanua kuwa, hata msala ambao ulimfikisha Rose korokoroni katika Kituo cha Polisi
cha Msimbazi Dar hivi karibuni siyo wa shilingi milioni 6 kama ilivyoelezwa awali bali ni sh. milioni 2 ambazo si yeye aliyezipokea bali ni mwanaume huyo.

Alieleza kuwa katika msala huo wa  milioni 2 alizodaiwa kuchukua na kushindwa kwenda kufanya shoo Mombasa, Kenya, staa mwenzake wa Injili, Jennifer Mgendi alidaiwa kujua kila kitu alikataa kwenda Msimbazi kumtoa Rose akidai kuwa hajui chochote.

Stella alifunguka: “Tofauti na watu wanavyojua, Nathan hakuwahi kuwa meneja wa Rose bali alikuwa ni msaidizi wake tu. Kwa hiyo si kweli kusema eti Nathan aliamua kumwacha mwimbaji huyo kwa kisingizio cha kukosa mwelekeo.

“Msada pekee wa Nathan kwa Rose ni kumlipia gharama za studio alipokwenda kurekodi kwa mara ya kwanza wakati Rose akiwa anasali Kanisa la Saint Mary, Chimuli, Dodoma. Ila kama mlivyiosema kwenye gaeri la Ijumaa (Wikienda) kuna mengi yapo nyuma ya pazia.

“’Ukichaa’ wa Rose ni pale alipokosea akaenda na Nathan, Cosota (chama cha hatimiliki) na kuingia makubaliano kwa maandishi kwamba huyo Nathan ndiyo awe analipwa mrabaha (sehemu ya mapato) ya kazi zote za Rose. Ni juzijuzi tu ndiyo Rose akaniagiza mimi nikamtengulie huo mkataba,” alisema katibu huyo ambaye pia ni mwimba Injili.

Aliendelea kufafanua kuwa mikataba yote ya kazi za Rose alikuwa akisaini Nathan hadi mwimbaji huyo alipochukuliwa na lebo kubwa ya Sony inayosimamia kazi zake kwa sasa.

Akaongeza: “Kama pesa yote ingekuwa inaingia mikononi mwa Rose asingekuwa hivi alivyop leo. Fikiria mpaka sasa Rose ana gari moja tu (Toyota Prado), viwanja 3 na shamba la eka 100 pale Dumila, basi (Morogoro).”

Kwa upande wake, Rose alisema kuwa Nathan alimfanya mashine ya kutoa na kuweka fedha benki (ATM).
Nathan alipoulizwa juu ya madai yote hayo alijibu kwa sauti yenye uhakika: “Hayo madai si ya kweli. Mimi nimeishi na Rose kwa zaidi ya miaka 12. Mimi ndiye niliyemsaidia yeye. Asingekuwa alivyo sasa kama si mimi.”
Credits:Global Publishers .

HUU NI UKATILI ULIOPITILIZA.

$
0
0

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mkazi wa Kijiji cha Nyabibuye Kakongo katika Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, Susuluka (16) anadaiwa
kujeruhiwa vibaya usoni na bosi wake, Imani Paulo (36) kwa kung’atwa ng’atwa usoni na kisha kunyofolewa macho, pua na meno kubaki nje, kama ambavyo anaonekana pichani.
Tukio hilo ambalo tunaweza kulifananisha na dunia kuelekea kufika mwisho, limegusa hisia za watu wengi hasa wakazi wa Kibondo, huku wengine wakitokwa na machozi kutokana na kuguswa na ukatili ambao amefanyiwa kijana huyo.Tunaweza kufikiria kuwa tukio hilo ni sinema, lakini Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Venance Mwamotto, ameliambia Majira kuwa tukio hilo limetokea miezi miwili iliyopita.
Akizungumza na Majira katika mahojiano maalumu, Mwamotto, alisema kuwa kabla ya kijana huyo kujeruhiwa na bosi wake, alimtuma dukani ili akamnunulie soda.Aliliambia Majirakuwa baada ya kufika nyumbani alimkuta bosi wake akiwa amemkaba koo mbwa na kutokana na maumivu aliyokuwa akiyapata mbwa huyo, alianza kuhema akitoa ulimi nje.
DC Mwamotto alisema kuwa mtuhumiwa huyo ghafla alianza kuung’ata ulimi wa mbwa na kisha kumeza vipande jambo lililosababisha mbwa huyo kupiga kelele kutokana na maumivu.Aliongeza kuwa aliendelea kula vipande vya ulimi huo wa mbwa hadi alipoumaliza.
“Unaweza kusema kuwa ni uongo, lakini ni tukio la kweli kabisa kwani mshtakiwa huyo aliendelea kula ulimi wote wa mbwa, huku kijana huyo akiendelea kumshangaa bosi wake kutokana na kitendo hicho kilichosababisha mbwa huyo kufa,”Wakati akiendelea kumshangaa bosi wake ghafla alimrukia na kumkamata kwa nguvu na kuanza kumng’ata kama mtu anayetafuna hindi la kuchoma.
“Mshtakiwa huyo alianza kumtafuna jicho moja na kufuatia jicho la pili na kisha kumeza vipande vya macho huku akiendelea kumshika kwa nguvu,” alisema DC Mwamotto wakati wa mahojiano naMajira.
Baada ya kumaliza kitendo hicho alisema kuwa mshtakiwa huyo alianza kumng’ata pua na kisha kumeza na vipande.
Alisema kuwa wakati anaendelea na kitendo hicho majeruhi huyo alikuwa akipiga kelele za kuomba msaada, lakini mshtakiwa huyo alianza kumng’ata tena kipande cha mdomo wa chini na kisha kusababisha meno kubaki nje.“Kutokana na kelele hizo wananchi waliamua kusogea karibu, lakini walikuta tayari, Susuluka amejeruhiwa vibaya usoni huku damu zikimtoka kwa wingi,” alisema.
Mwamotto alisema kuwa kutokana na hali hiyo wananchi walimvamia na kumpiga na kumpeleka katika Kituo cha Polisi cha Kibondo na majeruhi walimkimbiza katika Hospitali ya Wilaya ya Kibondo.
Majira iliendelea na mahojiano hayo ambapo, mshtakiwa huyo alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya na kufunguliwa mashtaka ya kudhulu mwili.“Hivi sasa mshtakiwa yupo katika Gereza la Nyamisivi Kibondo, lakini cha kusikitisha tena akiwa huko alimng’ata na kula vipande vya nyama vya mguu mshtakiwa mwenzake,” alisema.
Alisema kuwa mshtakiwa mwenzake alimjeruhi vibaya na kupelekwa hospitalini hali iliyosababisha mshtakiwa huyo kutengwa na washtakiwa wenzake.“Mimi nimelazimika kwenda hadi gerezani na kufanya mahojiano na mshtakiwa huyu, kwani hili tukio linasikitisha sana lakini cha ajabu alitaka kufahamu je ameshtakiwa kwa makosa gani ya kuua mbwa au kumng’ata mtu,” alisema.
Alisema kuwa pia amelazimika kwenda kumjulia hali majeruhi huyo ambapo madaktari katika hospitali hiyo walishindwa kumtibia.“Nimeomba msaada kutoka Wizara ya Afya ili mgonjwa 
huyu akatibiwe India na tayari maandalizi yameanza kufanyika kwa kushirikiana na Hospitali ya Kibondo,” alisema.
Mwamotto alisema kuwa mgonjwa huyo hana pua, macho yamefumba, mdomo kwa kujeruhiwa vibaya usoni hali ambayo anahitaji matibabu zaidi.Amewaomba Watanzania kumsaidia kijana huyo ili aweze kwenda kutibiwa haraka nje pamoja na kupata msaada mbalimbali kwa kuwasiliana na mganga mkuu wa hospitali ya Kibondo ama kuwasiliana 
Habari hii kwa hisani ya gazeti la majira la Tanzania. 

HII NDIO JEURI YA DIAMOND PLATNUMZ.

$
0
0

Wote tunajua kwamba diamond platnumz kwasasa anafanya kazi na coca-cola kama brand ambassador na Vodacom Tanzania pia.lakini chini ya kapeti hauwezi kuamini deals diamond anazozipata kila kukicha na kuzipiga chini. Diamond alifunguka hivi kuhusiana na hilo.


“Before mimi, wapo wasanii kibao walikua wakitumiwa na makampuni ya kibiashara,lakini maslahi ya kiuchumi hayakua makubwa kutokana na wasanii wenyewe kutojipa thamani. Ukiniona mie nimekubali kufanya kazi na makampuni ya kibiashara ujue lazima akaunti yangu imekaa vizuri sana. Naijua thamani yangu vizuri,i’ve worked hard kufika hapa nilipo and no one should take me for granted. Nashukuru mungu ubishi wangu umenisaidia nalipwa vizuri kama wasanii wengine barani afrika wanavyolipwa,though nimekua (Usisahu kulike page yetu mpya kwa kuclick HAPA)vilevile na lose sana,mfano hivi karibuni kuna kampuni moja ya simu ilinipa deal ya $200,000 but i turned it down coz walishidwa kufikia dau langu,also there was a deal na kampuni moja ya unga walitaka kunipa ubalozi , i told them to pay me $120,000 wakasuasua mpaka ilipotoka my number 1 wakarudi tena nikawaambia thamani yangu imepanda waongeze mtonyo na wakishidwa wafanye kazi na msanii mwingine kwa bajeti hiyo,haikua kwa ubaya it was a pure business. Ukweli ninastahili kulipwa fedha ninazowaambia kwasababu huwa nazifanya vizuri kazi zangu zote kibalozi na ndio maana coca cola wananitreat vizuri”.

Kanye West awatukana maDj wa radio kwa kuwataja majina kwenye tamasha.

$
0
0
Akiwa kwenye show aliyofanya huko Penn State, ikiwa ni muendelezo wa tour yake ya ‘Yeezus’, rapper huyo alisimamisha muziki wakati fans wakiwa wanashangweka na wimbo wake ‘Touch The Sky’ na ghafla akaanza kuporomosha matusi kwa madj wa wawili wa radio wanaofahamika kwa majina ya Charlamagne na Sway.
Kanye aliwachana kwa kuwataja majina kutokana na beef iliyokuwepo kati yao mwaka jana ambapo maDj hao kwa nyakati tofauti walikosoa tabia za rapper huyo na kumtaja kama mbinafsi na mwenye majivuno (egoistic and narcissism).
“If I go to a radio interview, SHUT THE F**k UP!!! ... Diss me, talk sh*t. What the f**k did you do? What have you done with your motherf**kin' life, Charlemagne? Sway?”
Lakini kama walivyosema kuwa ni mtu wa majivuno, akawapa na jinsi ambavyo ameweza kufanikiwa katika kipindi cha miaka kumi tangu aanze muziki akiwa Chicago.
“We in the studio every night. We get up at 5 A.M., we write nice s**t, working hard on that s**t, this ain't no joke. We think about nobody, we think about Shakespeare, we think about Beethoven, what can we make for y'all, what u playin' in y'all way to school on y'all way to work. What can we make to y'all feel better?”
Kuonesha kuwa aliyoyasema alikuwa aliyapanga tangu awali na ilibidi ayaweke yaingilie show kama matangazo muhimu, akajigamba kuwa yeye ndiye Yeezus na kisha akaamuru show iendelee, “that was the intermission now I will continue with the show.”
Matusi hayo yalimgusa Dj Charlamagne na akaamua kuweka ya moyoni kwenye mtandao wa kijamii wa twitter, akioneshangaa kwa nini Kanye ameamua kufanya hivyo wakati tayari imeshapita miezi minne tangu hayo yote yatokee mwezi October mwaka jana.
“I hope Kanye rants about me in every cit. Charla-MAYNE. Kanye’s first rant in months and its about me based off an interview that happened in October? That’s pretty dope.” Aliandika Dj huyo.

BABAMZAZI POOL CLUB LEO LIVE NA MASHUJAA POOL CLUB.

$
0
0

Babamzazi Pool Club ambayo ni Club Mpya Kabisa leo itachuana na Wakongwe na Mabingwa wa POOL Mkoa wa Ilala 2013/2014 Mashujaa kwenye Uwanja wao wa Nyumbani Vingunguti Mashujaa Pub.

Mechi hiyo ya shika nikushike itaanza saa 7 mchana mpaka 10 jioni.
Timu ya babamzazi inaundwa na Vijana Chipukizi na pia ni Timu mpya na mechi ya leo ndio Mechi yao ya kwanza.
Pamoja na kwamba ni timu mpya na inaundwa na Vijana Chipukizi ila kwa kujiamini wameahidi kutoa kipigo Cha paka mwizi kwa Wakongwe Mashujaa.
Makamu Mwenyekiti wa babamzazi Hussein Baha amesema baada ya Mashujaa wiki ijayo watacheza na Mpo Afrika iliyoko Tandika na Baada ya Hapo ni Top land ambao ndio Mabingwa wa Tanzania 2013/2014.
Kauli mbiu ya babamzazi pool club ni Hapa Kazi tu Hatufagilii Majina.
Wote Mnakaribishwa kushuhudia mpambano huo Mkali Pale Vingunguti Mashujaa Kuanzia saa 7 mchana.

DIVA WA CLOUDS FM AWEKA KILA KITU ADHARANI KUHUSU UHUSIANO WAKE WA KIMAPENZI YEYE NA GK

$
0
0

Diva Clouds fm anazidi kuvunja ukimya na kuweka wazi juu ya mahusiano yake na Msanii aliyekuwa
anaunda kundi la East Coast King Crazy GK baada ya hapo jana kutupia picha katika akaunt yake ya instagram na kufunguka.. 

Nanukuu Caption iliyo katika hiyo picha aliyoweka diva "have a Beautiful sunday... i gotta man to take care of... Ofcoz my GK.. love y'all .. and kasema kawa miss sana but he is busy with His Masters at Mzumbe Uni .. so love from US..



Mwanafunzi Mwaka wa Kwanza Ajinyonga Baada ya Kufeli Mitihani.

$
0
0
Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo cha Ualimu  cha Winneba, nchini Ghana, amejiua kwa kujinyonga mara baada ya jina lake kubandikwa kwenye ubao wa matangazo (notice board) kuwa amefeli masomo matatu.



Jina la mwanafunzi huyo limehifadhiwa kwa sasa, ila inasemwa kuwa sababu ya kujinyoga kwake ni kutokana na kufeli masomo hayo matatu ambapo kungepelekea kufutwa kwake shule hapo.

Sababu hasa ya kifo chake haijajulikana moja kwa moja ila inaaminika ilitokana na hofu ya kutimuliwa chuoni hapo kutokana na kufeli mitihani mitatu.

Wilson Dabuo, ambaye ni muwakilishi wa wanafunzi kwenye baraza la chuo hicho, alieleza kupitia Joy News kwamba chuo hicho kina sheria ya kutimua wanafunzi wanaofeli masomo matatu kwenye mitihani yao.

Hebu Angalia Kituko Alichokivaa Msichana Huyu Katika Ulimwengu wa Fasheni.

$
0
0
Je hii ni sawa, hivi kweli anaweza kukifanya hiki kama kivazi chake rasmi cha mtoko?

Kitu kimoja, kivazi hiki kimenifanya niufikirie huu ulimwengu wa fasheni na hawa wabunifu wetu, hata sielewi ni nini hasa huwa wanakaa na kufikiria kisha kuja na mitindo kama hii...

Lulu akiri mahakamani kuwa alikuwa na uhusiano wa mapenzi na Kanumba.

$
0
0

Kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabiri muigizaji wa kike, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu imesikilizwa leo (February 17) katika mahakama kuu, Kanda ya Dar es Salaam.

Lulu alikiri mbele ya Jaji Rose Temba kuwa alikuwa na uhusiano wa mapenzi na marehemu Steven Kanumba na kwamba walikuwa na ugomvi, lakini alikana mashitaka ya kumuua bila kukusudia.
Mbali na kukiri kuwa na uhusianano wa mapenzi, muigizaji huyo pia alikiri kuwa baada ya tukio hilo alitoka nje ya chumba walichokuwepo na kwenda kumwambia mdogo wake marehemu Kanumba, Setti Bosco kuwa Kanumba ametangulia mbele ya haki.
Akisoma hati ya mashitaka, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Monica Mbogo, alidai kuwa Aprili 7, mwaka 2012, Sinza Vatikani, Mkoa wa Dar es salaam, mshitakiwa alimuua bila kukusudia Stevin Kanumba.
Wakili Kombo, alidai kuwa pamoja na mambo mengine, marehemu Kanumba baada ya kufa, mwili wake ilipelekwa hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo majibu yanaonyesha kwamba kifo chake kimesababishwa na uvimbe ndani ya ubongo.
Upande wa serikali una mashahidi watano pamoja na vielelezo wakati upande wa utetezi pia unatarajia kuwa na mashahidi watano na vielelezo.

Mwanaume aliyempa ujauzito Lil Kim ajitokeza, ni rapper wa New York, ataja jinsia na mwezi watakaopata mtoto.

$
0
0

Wiki iliyopita mashabiki wa rapper wa kike na member wa zamani wa Junior M.A.F.IA, Kimberly Denise Jones aka Lil Kim walikuwa surprised baada ya rapper huyo kuweka wazi kuwa anaujauzito na kuonesha picha, “I can’t wait to be a mom”.

Lakini swali kubwa lililobaki kwenye mabano ni kuhusu jina ama kumfahamu baba mtoto wake ajaye, suala ambalo lilizua tetesi nyingi na majina mengi kutajwa kwa kubahatisha.
Hata hivyo majibu yamepatikana tayari ambapo rapper wa New York anayejulikana kwa jina la Mr. Paper amefunguka kwenye interview aliyofanya kwenye ‘The Rickey Smiley Morning Show’ kuwa yeye ndiye baba mtoto wa Queen Bee.
“Tuko pamoja. Kila kitu kiko poa. Huyo ni mke wangu na huyo ni mtoto wangu.” Alisema Mr. Papers na kuongeza kuwa Lil Kim ana ujauzito wa miezi takribani sita na kwamba wanatarajia kupata mtoto kati ya mwezi May au June.
Rapper huyo aliiweka wazi jinsia ya mtoto huyo kwa kutumia kiwakilishi cha jina kinachomaanisha kuwa ni mtoto wa kiume na kumsifia kuwa atakuwa ‘Gemini’, yaani mtoto aliyezaliwa katikati ya mwezi May na June lakini mbunifu na mwenye akili.
Hata hivyo hakutaka kutaja jina la mtoto walilolichagua, “ila tutawafahamisha wote hivi punde.”
Rapper huyo alikuwa katika mahusiano kwa muda mrefu na Lil Kim japo katika kipindi cha hivi karibuni hawakuwa wazi kuhusu kinachoendelea katikati.
Mwaka 2012, Lil Kim aliwahi kutweet kuwa yeye na rapper huyo wameachana, “As of 2night me & Papers are officially over. No malice or bad blood. I’ll see U guys soon #DaysofXmas.”
Paper naye akajibu akimwambia Lil Kim asishindane na nafsi yake, “@LilKim don’t be so mad you fighting with ya self…Get ya facts str8 lol.” Lakini baadae waliyamaliza na kurudiana, huku wakishirikiana kufanya Remix ya wimbo wa Rihanna ‘Pour It Up’, na kuonekana wote kwenye video ya wimbo huo iliyotoka mwezi March.

Mtaalam wa Saikolojia na uhusiano anaeleza sababu za watu kujiua au kuua kwa sababu ya mapenzi.

$
0
0

Bila shaka umewahi kusikia ama kwa bahati mbaya kushuhudia mtu aliyeamua kujitoa uhai ama kumtoa uhai mpenzi wake kwa sababu ya mapenzi.

Wapo wanaoandika ujumbe wa sababu zilizopelekea yote yatokee baada ya kushindwa kuvumilia mabaya na maumivu ya penzi walilotarajia lingekuwa tulizo la moyo wao.
Sylvester Paul, yeye ni mtaalam wa saikolojia na mahusiano, mtanzania aliyesomea mambo hayo nchini Afrika Kusini na baadae kurejea nchini ambapo ameweza kuandika vitabu kadhaa vinavyohusu mahusiano ya mapenzi, kama vile ‘Moyo Ulioumizwa Kimapenzi’, ‘Mtambue Mwanamke’, na vingine.
Mtaalam huyu ameelezea sababu za kisaikolojia zinazopelekea mtu kuamua kujiua ama kumuua mwenzi wake chanzo kikiwa mapenzi:
“Watu wanakufa kwa sababau Love imekamata uhai wa mtu, ambao unaitwa soul au nafsi. Sasa nafsi imegawanyika katika sehemu tatu, kwenye nafsi kuna mind, kuna emotion na kuna will. Kwa hiyo love ile inaendaga kwenye mind ambayo ni ufahamu, inamvuruga mtu kabisa. Baadae inatoka kwenye ufahamu inaenda kwenye emotion (hisia), mtu anaanza kufanya vitu sasa vitendo. Hapakaliki ofisini, kachanganyikiwa, yaani maisha yote yanakuwa magumu kwake, sometimes anashindwa kulala.
“Ikishatoka kwenye ufahamu, inaenda kwenye ‘will’, yaani nguvu ya maamuzi, unakuta mtu sasa anachukua gari anaanza kusafiri. Mpaka mtu anafikia hapo ujue ameshaumia, love imeshamtesa sana kwenye ufahamu, ikaenda kwenye ufahamu hadi kwenye nguvu ya maamuzi. Kwa hiyo akaamua ku-sacrifice.
“Sasa kinachoweza kumfanya mtu amuue mtu mwingine, ni kwa sababu amekubali kutoa upendo wake na maisha yake na mtu mwingne. Love ni kugawana maisha, wewe hamsini, mimi hamsini. Na ndio maana tunasema Love is a strong feeling of deep affection. Ina maana huyu mtu tayari ameshakuwa affected, ameathirika kisaikolojia, ameathirika katika mambo yote, spiritually na mentally huyu mtu amekufa.
“Vitabu vingine vinasema love is stronger than death, upendo una nguvu kulio mauti. Unaposaini kumpenda mtu umesaini na kifo. Ndio maana tunasema love is stronger than death. Yaani unapompenda mtu umeunganisha na kifo.
“Ukiingia kwenye love umeingia kwenye agano, ndio maana mtu anasema nimekufa kwa ajili yako. Halafu wewe leo unaenda kumbemba mtu ambaye nimekufa kwa ajili yake.
Chanzo: Kipindi cha Sun Rise cha 100.5 Times Fm.

Filamu aliyoigiza Ben Pol 'Sunshine', kuzinduliwa February 20, Ben Pol amsifia Bi Kiroboto.

$
0
0

Filamu aliyoigiza mwimbaji wa RnB, Ben Pol na mchekeshaji maarufu, Bi Kiroboto, iliyoandaliwa na kamupni ya Swahilihood itazinduliwa rasmi February 20 mwaka huu.

Mratibu wa Swahilihood, Hassani Mrope ameiambia tovuti ya Times fm kuwa filamu hiyo ya Sunshine itazinduliwa pamoja na filamu nyingine mbili ambazo ni ‘Mdundiko’ na ‘Network’. Filamu hizo zitazinduliwa kuanzia saa kumi na mbili jioni, Century Cinemax, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Nae Ben Pol aliingelea filamu hiyo katika kipindi cha The Jump Off cha 100.5 Times Fm na kumsifia muigizaji huyo wa kike aliyecheza nae kama mama yake, Christina Mbunda aka Bi Kiroboto.
Mwimbaji huyo alieleza kuwa mbali na kuigiza vizuri kama mama mwenye moyo mzuri anayejali familia yake, hata katika uhalisia ni mama bora anayejali.
“Yaani mimi nimeienjoy sana, nilikuwa nafeel kama ni mama yangu mzazi”, alisema Ben Pol.
“unajua bi Kiroboto, ukitoa upande wa kazi wa kuigiza, yaani ni mama mmoja very humble. Yaani ni mama…anaiele feeling ya mama ile…unajua hata kama mko kwenye set kichwa kinauma au nini, yaani ana ile care ya mama. Yaani mpaka nammiss.” Aliongeza Ben Pol.
Kwa mujibu wa Ben Pol, filamu hiyo ilishutiwa kwa muda wa mwezi mmoja.

MCHAWI WA UNGO ADONDOKA, AGEUKA KUKU.

$
0
0
HALI ya taharuki iliyoambatana na imani za kishirikina iligubika Jiji  la  Arusha kufuatia mwanamke ambaye hakufahamika jina kudondoka na ungo wa kishirikina
asubuhi ya Ijumaa iliyopita kisha ghafla kubadilika  kuwa kuku mweupe mwenye mayai ndani ya ungo, Uwazi limeona mengi.

Mamia ya wananchi katika eneo la Kimandolu kando ya Barabara ya Arusha- Moshi walimiminika kushuhudia tukio hilo lililojiri saa tatu asubuhi.

Akizungumza na Uwazi, shuhuda mmoja wa tukio hilo ambaye ni dereva wa bodaboda, Martin Mbise alisema:
“Nilikuwa kwenye shughuli zangu za kila siku, ghafla niliona kitu kipana kikidondokea kwenye huu mtaro, ndani yake nikamwona mtu amekaa akiwa uchi wa mnyama.

“Wengi tuliamua kusogelea eneo la tukio, lakini kabla hatujakifika, mtu huyo alitoweka, badala yake mle mwenye ungo  mkawa na kuku mweupe na mayai zaidi ya kumi, tulishangaa sana:
Mbise alisema hali hiyo ilidumi kwa saa mbili na nusu, ndipo wananchi hao wakaamua kumchoma moto kuku huyo baada ya kumuua na kuyavunja mayai.

Hata hivyo, alisema haikuwa rahisi kuku huyo kuungua licha ya kumwagiwa mafuta ya taa na petroli na wakachukua uamuzi wa kumkatakata na kugawana nyama yake huku baadhi
yao wakikimbia hovyo na kulaani tukio hilo.

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo walisema tukio hilo ni laana na anapaswa kuitwa mtumishi wa Mungu kwa ajili ya kukemea pepo mchafu kwa maombi ya kiroho wakiamini mchawi huyo alikuwa ana lengo la kuwadhuru.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Lebaratus Sabas hakuweza kupatikana kuzungumzia tukio hilo, lakini baadhi ya maafande waliofika katika eneo hilo walithibitisha. 
Viewing all 2632 articles
Browse latest View live