Kwa kuzingatia hilo, mwimbaji wa kike ambaye pia ni muigizaji wa filamu za Kiswahili, Shilole aka Shishi Bybee, alipiga story na tovuti ya Times Fm katika kipengele cha Times Q & A, na kuelezea sifa za mwanaume ambaye atafaa kuwa mumewe wa ndoa.
“Mimi nampenda mwanaume mchapakazi, anayempenda Mungu. Mwanaume mweusi, mwembamba lakini asiwe mwembamba sana…kawaida.” Shilole amefunguka.
Hata hivyo, Shilole ambaye ana watoto wawili amesema kuwa kwa sasa hana mpango wa kuolewa.
“Watoto tayari ninao wawili, sina mpango wa kuolewa. Kuolewa ni maamuzi ila bado sijaamua, nikiamua ntaolewa tu.”
Shilole ambaye mwaka jana alifanikiwa kupata show nchini Uingereza, ameachia wimbo wake unaoitwa ‘Chuna Buzi’ na mashabiki wa muziki wake wanaonesha kuulewa.
Credit:Times fm