
Tarehe 1 April 2014 Best New Ticket imefanya utafiti kugundua album ipi ina maneno machafu zaidi toka mwaka 1985 mpaka mwaka 2013 na kugundua kuwa album ya marehemu 2 Pac ‘All EyeZ On’ ndio album inayoshika namba moja kwa maneno na lugha chafu zaidi.
Utafiti huu umeangalia album 2,296 za muziki wa rap zilizotoka kuanzia mwaka 1985 mpaka mwaka 2013. zinazochaguliwa kwa mauzo bora, ukubwa wa jina la msanii na jinsi album ilivyopokelewa na wateja sokoni.
Album mbili za Tupac, 2Pacalypse ya mwaka 1996 na All Eyez On Me imekutwa na lugha chafu ikiwaimetumika mara 901, matusi ni asilimia 33.52 kwenye wimbo mmoja na neno Nigger likitajwa mara 404. Asilimia 44 ya matusi kwa album yote.
Kweney All Eyez On Me yenye cd mbili na nyimbo 27 nayo ina lugha chafu zaidi, Album ya Notorious B.I.G. Ya mwaka 1997 ‘Life After Death’ yenye nyimbo 23, lugha chafu imetumika mara 615, matusi ni asilimia 26.73 kwa wimbo mmoja.