
Mwaka 2014 umeanza na mabadiliko kwa tajiri mkubwa zaidi Afrika, Aliko Dangote aliyeamua
kujiunga na mtandao kwa kijamii wa twitter ili aweze kufanya mazungumzo na watu wengi duniani kwa wakati mmoja.Dangote aliandika ujumbe wa kwanza January Mosi akiwatakiwa watu wote heri ya mwaka mpya.
Akiwa ameandika tweets mbili tu hadi leo (January 4), ameshapata followers zaidi ya 36,500. Na ameahidi kuendelea kufanya mazungumzo na watu kupitia mtandao huo kadri anavyoweza.