
Producer mwenye rekodi ya kufanya kazi na wasanii wa kubwa duniani kama Jay Z, The Game na Justin Timberlake amechaguliwa kuwa mtayarishaji/muongozaji wa utayarishaji wa album mpya mpya ya Marehemu Michael Jackson.
Kwa Mujibu wa Jarida la Rolling Stone, Album hii inayotoka May 13 2014 itaitwa “Xscape” na tayari orodha ya watayarishaji imetolewa. Producers watakao husika ni Rodney Jerkins, Stargate, Jerome “Jroc” Harmon na John McClain.
Sauti ya Michael Jackson aliyefariki mwaka 2009,itapewa uhai na nyimbo nane zilizowahi kurekodiwa wakati wa uhai wake ila hazikupata nafasi ya kumaliziwa ili zitoke, hii ni kwa mujibu wa Chairman na C.E.O Wa Epic Records L.A. Reid,
“Michael ameacha kazi nzuri sana kwa dunia kuburudika nazo na tuna furaha kupata nafasi ya kuzitoa kwa watu” Alisema Raid.