
Rooney ambaye ameichezea timu hiyo tangu mwaka 2004, atakuwa anapata kitita cha pound 300,000 kwa wiki, sawa na dola 500,000 ni hivyo kuwa mchezaji wa ligi kuu ya Uingereza (EPL), anayelipwa fedha nyingi zaidi.
Kwa mujibu wa ripoti kutoka Uingereza, mkataba huo utakapoisha inaweza kuwa ndio wakati ambapo mchezaji huyo atakakuwa anastaafu soka na kwamba atabaki kuwa katika benchi la ufundi la timu hiyo.