
Tajiri huyo wa mashairi na flow ametweet ujumbe huo wakati akijibu tweet ya Oscar Maboko aliyoeleza kuwa albam hiyo iliuza nakala milioni kadhaa lakini iliathiriwa na wizi za kazi wasanii.
"#MachoziJashoNaDamu is an indisputable/classic/dope/great&prolly the best album of the 1st century! #PROFJ @OscarMaboko @africanhiphop." Ametweet Fid Q.
Katika hatua nyingine, mdau huyo wa muziki, Oscar Maboko alieleza kuwa anaamini hata albam ya kwanza ya Sugu enzi hizo anaitwa 2 Proud iliathiriwa kimauzo na kanda za kurekodi kwenye Fm Radio zilizokuwa zinauzwa mtaani na kwamba karibia kila kijana aliyekuwa na radio cassette alinunua nakala hizo.