
Utafiti wa wataalamu hao unaonesha mbwa anaweza kugundua saratani ya Tezi ya shingo ya binadamu (Thyroid) kwa kunusa tu, ambapo katika majaribio waliyofanya imeonekana 88% ya watu waliogundulika na mbwa walionekana kuwa na saratani hiyo baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kitaalamu.
Mbwa aina ya frankie kutoka Ujerumani alifundishwa kunusa mikojo ya watu wenye ugonjwa huo na majibu kuonesha kuna asilimia kubwa mbwa huyo anaweza kugundua watu walioathirika na cancer hiyo.
Wanasayansi wanaona kwa hii njia mpya huenda ikayasaidia maeneo mbalimbali duniani ambayo hayana vifaa vya kupimia ugonjwa huo.
Credit:Millardayo!