Quantcast
Channel: D'JARO ARUNGU
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2632

Askari Watatu Wajeruhiwa kwa Bomu Songea, Ruvuma

$
0
0


Askari Polisi wakiwa eneo la tukio kuimarisha ulinzi
Eneo la tukio  likiwa limezungushiwa alama na Jeshi la Polisi.Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwangu akizungumza jambo na waandishi wa habari katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma baada ya kuwatembelea majeruhi hao. Kamati ya ulinzi na Usalama wakiwa Hospital ya mkoa wa Ruvuma.Aliye lala kitandani ni WP ambaye amejeruhiwa akiwa amelazwa katika hospital ya Mkoa wa RuvumaMganga mkuu wa Hospital ya Mkoa wa Ruvuma Dr Daniel Malekela akizungumza na waandishi wa habari hopitalini hapo.Askari Ramadhani Ally akiwa anaelezea jinsi mkasa huo ulivowakuta wakiwa kazini
 
ASKARI watatu  wa jeshi la Polisi wamelazwakatika Hospitali ya Mkoa  wa Ruvuma  (Homso) iliyopo mjinisongea Mkoani humo  wakiwa wanapatiwa matibabu ya majeraha ambayowaliyapata baada ya kushambuliwa kwa kitu kinachodhaniwa kuwa ni Bomu lakurushwa kwa mkono.
 
Tukio hilo limetokea  September 16, 2014majira ya saa moja na nusu jioni katika kata ya Msufini karibu na daraja la Matarawe, wilayani Songea Mkoani Ruvuma  ambapo watu watatu wasiofahamika walitupa kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu la kutupwa kwa mkonoambalo limetengenezwa kienyeji na kuwajeruhi askari  hao watatuwaliokuwa doria.
 
Askari hao waliojeruhiwa ni  WP. 10399 PCFelista aliyejeruhiwa mguu wa kulia  kwenye unyayo na pajani  ,G.7351 PC Ramadhani aliye jeruhiwa mguu wa kulia karibu na goti na tumboni upandewa kulia na  G. 5515 pc John aliyepata majeraha katika mguu wa kuliachini ya goti na jeraha dogo tumboni.
 
Mganga mkuu wa Hospital ya Mkoa wa Ruvuma Dr. DanielMalekela ameeleza kutoa vipande vya bati na misumari katika majeraha ya askarihao na mpaka sasa wanaendelea na matibabu.
 
Alisema kufutia hali hiyo Jeshi la Polisi mkoaniRuvuma linaendelea na uchunguzi  wa kina ili kuwakamata wahusika watukio hilo kwa hatua zaidi za kisheria. 
 
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe. Saidi Mwambungu kasema  amesikitishwa sana na kitendo hicho cha wahalifu kujeruhi askari tena kwa makusudi na amesema serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama watahakikisha wanawasaka na kuwakamata.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 2632

Trending Articles