Quantcast
Channel: D'JARO ARUNGU
Viewing all 2632 articles
Browse latest View live

Article 0

$
0
0
 Kwa mara nyingine tena katika kipindi cha wiki mbili, winga machachari wa klabu ya Yanga Mrisho Khalfan Ngassa amemsifia mshambuliaji wa timu mahasimu Simba Mburundi Amiss Tambwe.

Akitumia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter Mrisho Ngassa alimsifia Tambwe kwa kumuita mshambuliaji bora. Hatua hiyo ya Ngassa ilikuja baada ya Tambwe kufunga mabao mawili katika mchezo wa jana dhidi ya Ruvu Shooting uliopigwa uwanja wa taifa na Simba kutoka na ushindi wa 3-2.

MUACHE MUNGU AITWE MUNGU,WATU WALIOMDHIHAKI ONA YALIYOWAKUTA.

$
0
0
1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)
Wakati alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American alinukuliwa akisema hivi"Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. Mafundisho ya Yesu yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle). Ilikuwa mwaka 1966.
Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki.

2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)

Alisema kwamba endapo angepata kura laki tano kutoka katika uchaguzi mkuu wa Brazil na kuwa rais, hata MUNGU asingeweza kumtoa katika urais huo. Akafanikiwa, akapata kura zaidi ya hizo, akashinda uchaguzi, siku moja kabla ya kuapishwa, akafariki dunia.

3. CAZUZA (MWANAMUZIKI WA BRAZIL)

Alipokuwa katika shoo yake ndani ya jiji la Rio De Janeiro, alichukua sigara, akaanza kuivuta, akachukua nyingine na kisha kuirusha juu na kusema "Mungu, hiyo yako, chukua nawe uvute"

Alifariki akiwa na miaka 32 kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ambayo iliyaharibu sana mapafu yake kuliko mgonjwa yeyote yule.


4. MTENGENEZAJI WA MELI YA TITANIC.

Baada ya kutengeneza meli ya Titanic, mwanahabari akamuuliza ni kwa kiasi gani ilikuwa salama nae akajibu "Ni salama sana, haiwezi kuzama na hata Mungu hawezi kuizamisha"
Nafikiri unajua kilichotokea kuhusu Titanic.

5. BON SCOTT (MUIMBAJI)

Mwimbaji huyu ambaye alitamba miaka ya 70 alitoa wimbo wake mmoja mwaka 1979 wenye maneno haya
"Don't stop me; I'm going down all the way, down the highway to hell'.

Tarehe 19 February mwaka 1980, alikutwa amekufa baada ya kupaliwa na matapishi yake.


6. Mwanamke mmoja alikuwa akihofia sana kuhusu ulevi wa marafiki wa mtoto wake. Wakati wanataka kuondoka na gari, akamshika mtoto wake mkono garini na kumwambia "Binti yangu, Mungu awatangulie katika safari yenu" Yule binti akajibu "Gari imejaa mama, huyo Mungu labda akae kwenye boneti la gari".


Baada ya masafa fulani ya safari yao, gari lile lilipata ajali kiasi ambacho hata polisi hawakujua ni aina gani ya gari lilikuwa.


Lilikuwa limebondeka sana na watu wote walikutwa wamekufa. Kilichowashangaza polisi, trey la mayai wala halikuonekana kuguswa na hakuna hata yai moja lililokuwa limevunjika na wakati gari lilibondeka mpaka kutokutambulika.


7. CHRISTINA HEWITT (MWANDISHI WA HABARI)

Huyu alikaririwa akisema hivi "Nimesoma vitabu vyote duniani, ila hakuna kitabu kibaya...kibaya na kibaya kama Biblia"
Siku chache baada ya kusema maneno hayo, mwili wake ulikutwa umeunguzwa na moto ambao haikujulikana mpaka leo ule moto ulisababishwa na nini.

8. MARILYN MONROE (MUIGIZAJI)

Huyu alifuatwa na Bill Graham na kumwambia kwamba alitumwa na Roho wa Mungu kwa ajili ya kumhubiria. Alimkaribisha ndani, akamsikiliza kwa makini, alipomaliza akasema "Simhitaji Yesu wako, unaweza kuondoka nae". Wiki moja baadae, alikutwa amekufa katika makazi yake. Polisi walijaribu kuchunguza kipi kilimuua, mpaka leo hawajapata jibu.

KIJANA ALIYEGEUKA ALBINO BAADA YA KUATHIRIKA NA MATUMIZI YA MADAWA AINA YA METAKELFIN.

BABA MZAZI POOL CLUB MABINGWA WA BONANZA MKOA WA DAR ES SALAAM 2014.

$
0
0
Hongera kwa Timu ya Pool ya Baba Mzazi,Jana Wameonyesha Ubabe Dar Live kwa kuwa Bingwa wa Bonanza la Mwezi ambapo Timu Kibao za Dar es Salaam na 1 ya Moro iitwayo Anatory.

Babamzazi ni Timu Changa sana na hiyo ndo ilikuwa Bonanza lake la Kwanza ambapo aliwatoa Jasho Mabingwa wa Pool Tanzania.

Kabla ya hapo wiki 2 zilizopita ilicheza na Mashujaa katika uwanja wake wa Nyumbani na Kuwafunga 13 kwa 11.

Timu zilizokuepo jana ni pamoja na Mabingwa wa Tanzania Topland,Mabingwa Wa MOROGORO Anatory,Mabingwa wa Ilala Mashujaa nk.

Zilikuepo pia timu za Kinondoni kama Silva na Mkwajuni lakini zote zilikalishwa na babamzazi pool club.
Jumapili hii ya tarehe 9/03/2014 itacheza mechi ya Kirafiki na Top Land katika Ukumbi wa Mshujaa Vingunguti.Mechi itaanza saa 9 alasiri.





WEMA AMHARIBIA PASTOR MYAMBA.

$
0
0

STAA wa filamu mwenye jina kubwa nchini, Wema Sepetu hivi karibuni alimuharibia siku Emanuel
Myamba maarufu kama Pastor Muyamba, kwa kushindwa kufika kwenye hafla iliyokuwa imeandaliwa na chuo chake cha sanaa ‘TFTC’ akiwa kama mgeni rasmi.

Mtoa habari wetu ndani ya taasisi hiyo aliliambia gazeti hili kuwa, Wema aliombwa na kukubali kuhudhuria shughuli hiyo, lakini alipopigiwa simu dakika za mwisho aliwaambia kwamba atashindwa kufika kwa kuwa amefiwa na shangazi yake udhuru ambao baadaye ulibainika kuwa haukuwa wa kweli.

Alisema kutokana na kutofika kwa staa huyo, ambaye hata hivyo mwaliko wake ulitokana na shinikizo la wanafunzi wa chuo hicho, walilazimika kuwaomba radhi wageni wengine, wakiwemo waandishi wa habari.

Mmoja wa watu wa karibu na Wema aliliambia gazeti hili kuwa muigizaji huyo hajawahi kupatwa na msiba siku za hivi karibuni, kwani mara zote amekuwa akiwaeleza kila linapotokea jambo zito kama hilo.

Mtu huyo alisema katika ratiba ya siku hiyo, walikuwa waende kwenye tukio moja la starehe na halikuwa limebadilika.

juzi alipoulizwa Pastor Myamba alikiri Wema kutofika kwenye hafla hiyo kitendo alichosema kimemsikitisha kwani walitoa mwaliko kwake kutokana na heshima aliyonayo.

“Nimemshangaa sana, lakini mbona mwenzake Jokate alikuja, ni kwa sababu anajitambua na ni professional,” aliema Myamba.
Credit:GPL

>>Gonga Like Yako Hapa Kwa Mastory Kibao>>

Maskini Mtoto Huyu Mlemavu.

$
0
0
Moshi Hussein ambaye ni mlemavu wa viungo anayeishi nyumbani kwa baba yake mzazi huko katika kijiji cha Magiri wilaya ya Uyui mkoani Tabora,binti huyu ana umri wa miaka 13 hajawahi kupelekwa Shule kwa maana ya kupata haki kama wapatavyo watoto wengine,Moshi amekuwa akililia hilo kwa baba yake mzazi bila mafanikio.Jambo baya zaidi kwa mujibu wa maelezo ya Moshi baba yake anahitaji aolewe ili aweze kupata Ng'ombe licha ya kuwa ana umri mdogo na hawezi kukabiliana na Changamoto za ndoa kulingana na ulemavu alionao.
Moshi kwakuwa hana uwezo wa kutembea umbali hata wa hatua kumi anawaomba wasamalia wema kumsaidia mambo makubwa matatu,kwanza ikibidi kumuondoa nyumbani kwao ili aepukane na ndoa ya lazima,Pili apelekwe shuleni kwakuwa anaona kukaa kwa baba yake ni wazi kwamba atakuwa anatafuta umasikini mwingine wa ziada ukiachana huo wa ulemavu wa viungo ambao umekuwa kikwazo kikubwa hata cha kujihudumia masuala mengine ya kiutu wa mwanamke.Kwa mujibu wa maelezo yake Moshi ana mshangaa baba yake kwa uamuzi wa kutaka aolewe kwakuwa hata ndoa yenyewe haoni kama itakuwa na maana kutokana na ulemavu alionao na pia haoni sababu ya kuwa mzigo kwa mtu mwingine katika maisha yake.
Moshi amekuwa akijikatia tamaa kulingana na ulemavu alionao,"Kama ningekuwa na mama labda hata ningeweza kupelekwa shule na mimi ningekuwa msomi kama wengine,lakini kwa hali hii ni bora hata ningekufa nimfuate mama yangu huko aliko"
Via KapipiJHabari
>>Gonga Like Yako Hapa Kwa Mastory Kibao>>

Nikki wa Pili asema 'Weusi' imemsimamisha kazi Lord Eyez

$
0
0
Msemaji wa kundi la Weusi, Nikki wa Pili amesema kuwa rapper Lord Eyez amesimishwa kazi katika kampuni hiyo na kwamba kwa sasa sio ‘member’.

 “Kitu ambacho naweza kusema kutoka Weusi ni kwamba Lord Eyez tumemsimamisha kazi kikampuni.” Amesema Nikki wa Pili na kusisitiza kuwa hajafukuzwa kazi bali amesimamishwa.
Hata hivyo, Nikki wa Pili hakuwa tayari kuweka wazi moja kwa moja sababu zilizopelekea Weusi kumsimamisha kazi rapper huyo.
“Hizo ni confidential, ni issue za kampuni hatuwezi kuziweka wazi lakini Lord Eyez tumemsimamisha kazi hiyo ndio taarifa ambayo tunaitoa kwa media.” Nikki wa Pili ameeleza.
Ameongeza kuwa kwa sasa matukio yote yanayotokea kwa upande wa Lord Eyez yatakuwa yanamhusu yeye binafsi na hayatakuwa na uhusiano wowote na kampuni.
Hii inamaanisha hivi sasa Weusi inaundwa na Joh Makini, Nikki wa Pili, G-Nako na Bonta.
Uamuzi huo wa Weusi umekuja wakati ambapo kumekuwa na taarifa kuwa Lord Eyez alikamatwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za wizi Jumamosi, huko Arusha na baadhi ya picha za tukio hilo kuonekana. Taarifa hizo zimedai kuwa anatuhumiwa kwa wizi wa laptop aina ya 'Dell'.
Mwaka juzi, Lord Eyez alikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za wizi wa Power Window za gari la Ommy Dimpoz, lakini Ommy alitangaza kumsamehe msanii huyo.
Weusi walichukua dhamana ya kumtetea na kumuwekea mwanasheria huku wakifanya mikutano na waandishi wa habari ili kuitengeneza image ya kampuni hiyo ambayo ilikuwa imewekewa alama na tuhuma za Lord Eyez ambaye ni member wa kundi la Nako 2 Nako.  

Arnold Schwarzenegger kuanza kushuti toleo jipya la 'Terminator', kucheza kama Cyborg.

$
0
0

Akamuomba Jaji amrudishe jela miezi sita ili akamalizie kozi yake, adai itamsaidia kwa maisha ya baadae

$
0
0

Maajabu!! Shuhudia Chatu Alivyomshinda Mamba Nguvu Australia Kisha Kumla.

$
0
0

MASKINI RAY C AMUONEA HURUMA MPENZI WAKE WA ZAMANI.

$
0
0

RIDHIWANI KIKWETE AULA CHALINZE,ASHINDA KURA ZA MAONI CCM.

$
0
0

Matokeo:
Ridhiwani Kikwete kashinda kwa kupata kura 758 kati ya kura 1321.

Ilikuwa hivi:_
1.Ridhiwani Kikwete kura 758
2.Shaban Iman Madega kura 335
3.Athuman Ramadhan Maneno kura 206
4.Changwa Mohamed mkwazu kura 12
Kura zilikuwa 1363 zilizo Haribika 5 na Halali ni kura 1316
Wagombea wa Ubunge Chalinze kwa tiketi ya ccm walikuwa ni:-
1.Ndg.Ridhiwani Kikwete,
2.Shaban Iman Madega,
3.Athuman Ramadhan Maneno
4.Changwa Mohamed mkwazu

Tarehe 9/3/2014 KUCHUKUA FOMU
Tarehe 11/3/2014 KURUDISHA
Tarehe 15/3/2014UZINDUZI RASMI WA KAMPENI ZA CCM

CHANZO JAMIIFORUMS

BAADA YA PNC OSTAZ JUMA AMGEUKIA HUYU MSANII WA BONGO MOVIE.

$
0
0
 Haya Baada ya lile Saga la PNC kumpigia Magoti Ostaz Juma sasa Amekuja na hii mpya ya Kusema
Johari Hawezi hawezi kumsahau Ostaz katika Maisha yake siri anayo yeye ...Mhhh Siri Gani hiyo ? 


MDOGO WAKE MAREHEMU KANUMBA ADAI KANUMBA ANAMTOKEA.

$
0
0
SETH Bosco aliye mdogo wa marehemu Steven Kanumba, aliyekuwa staa wa filamu za Kibongo, ameibuka na kueleza mambo ya kushangaza, akidai kaka yake huyo amekuwa akimtokea.


Seth ndiye msimamizi na mwendeshaji wa Kampuni ya Kanumba The Great Film baada ya kifo cha Kanumba kilichotokea Aprili 07,2012 nyumbani kwake, Sinza – Vatican, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari hizi, wikiendi iliyopita jijini Dar es Salaam, kwa sauti ya huzuni, Seth alisema: “Kiukweli sina amani, hii hali inanitesa sana. Kila mara ananitokea ndotoni na kunieleza mambo yanayofanana.”

MAMBO GANI?
“Analalamika kwa nini eti ofisi yake aliyoiacha haina mafanikio. Sasa nashindwa kuelewa, ni mafanikio gani anayozungumzia. Analalamika kwa nini filamu hazitolewi, ni jambo la kweli lakini lipo nje ya uwezo wangu,” alisema Seth.

AMANI: Anakutokea kivipi yaani?
SETH: Nikiwa usingizini, nakuwa kama naota, lakini mazungumzo yanakuwa ya moja kwa moja... ndoto ikikatika, nashtuka na kujikuta nahema kwa kasi.

AMEMTOKEA MARA NGAPI?
“Mara ya tatu sasa, ndiyo maana nimeshindwa kuvumilia. Kinachonishangaza ni kwamba, kila anaponitokea, lazima nishtuke mwishoni na lazima niheme kwa kasi na kutoka jasho jingi.
“Mwanzoni nilichukulia kawaida, lakini alivyonijia mara ya pili na ya tatu nikaona hili suala siyo la kulikalia kimya, ikabidi nimwambie mama.”

MAMA KANUMBA ANASEMAJE?
“Mama alishtuka na ameshangazwa sana na hali hiyo. Ameniuliza imenitokea mara ngapi, nikamwambia tatu, akasema lazima tufanye maombi kuondoa hali hiyo,” alisema Seth huku akionesha uso wa wasiwasi.
Credits:Global Publishers

SHILOLE: BABY MADAHA HAJIELEWI.

$
0
0

STAA wa Mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amemfungukia msanii mwenzake, Baby Joseph Madaha kwamba  hajielewi.


Shilole ametoa kauli hiyo siku chache baada ya kuchanwa gazetini na Baby Madaha kwa kuambiwa kuwa yeye ni mcheza vigodoro.

“Sitaki kabisa kumsikia huyo Baby Madaha, hanisaidii chochote kile katika maisha na kazi zangu pia sioni sababu ya kupigizana naye kelele, mtu mwenyewe hajielewi,” alisema Shilole.

Nay wa Mitego kufanya collabo na Jose Chameleone.

$
0
0
Tushasikia uwepo wa collbao ya Steve RnB na Wyre Da Love Child iko jikoni, wakati Madee alishaitoa collabo yake na P-Unit wa Kenya, Chid Benz na Cannibal na bado orodha inaendelea.
Rapper wa Manzese, Nay wa Mitego amesema kuwa amepanga kufanya wimbo na mwanamuziki wa Kitamataifa, Jose Chameleone.
“Next Collabo…namatarajio ya kufanya ngoma na Chameleone.” Amesema Nay wa Mitego. “Bado haijakamilika, tuko kwenye Process.”
Katika hatua nyingine, Nay amesema kuwa project yake na Diamond ndio itakayofuata hivi karibuni, “soon as possible ngoma itaenda hewani.”

Iyanya asema anahangaikia pesa sio mapenzi, adai mapenzi bila pesa yanakufa.

$
0
0

Ulishawahi kuona filamu nyingi zikionesha hali ya kuwa na mapenzi ya kweli pale ambapo msichana mrembo na anayetokea kwenye familia tajiri akimpenda fukara? 


Bila shaka ndio. Lakini hii kwa Mkali wa Kukere, Iyanya haina uhalisia kabisa.

Iyanya ameliambia gazeti la iCampus kuwa kwa hivi sasa ‘status’ yake haieleweki na mara kwa mara inakuwa inabadilikabadilika, leo anakuwa kwenye mahusiano na kesho anakuwa single.
Hii imempelekea kuwaza zaidi kutafuta pesa kwa kuwa ameshashuhudia uhusiano wa watu wengi ukifa kutokana na ukosefu wa ‘chapaa’.
Iyanya amedai kuwa anahitaji kuwa na pesa na kujenga nyumba kama 20 jijini Lagos, na nyumba nyingine London, uingereza ili watu wakimsema sana Naija anaenda London kwenye mjengo wake kuchill.
Hivi ndivyo alivyoeleza Iyanya kwa lugha ya kiingereza ila kwa swag ya Naija:
 “Oh boy, it’s the two these days. Sometimes I am single; sometimes I’m in a relationship. You fit see me tomorrow and I go tell you say, “Oh boy, I don break up oh.” I fit wake up say I no do again. Then next tomorrow, I can be in a relationship. The thing just dey fluctuate. It’s not a do or die thing. Relationship isn’t what I’m after right now, I’m after the money. My problem is to make money and have like 20 houses in this Lagos – Island and Mainland. I want house for London, everywhere, so when people talk too much, I go just comot go my house for London go chill. How many relationship dey last without money? I’m just a natural guy. I’m a real Gee.”

KUTANA NA MWANAMKE MKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI.

$
0
0
Misao Okawa, ambaye aliwekwa kwenye kitabu cha rekodi kubwa za dunia ‘Guinness’ mwaka jana kama mwanamke mwenye umri mkubwa zaidi
duniani, jana (March 5) amefanya sherehe ya siku ya kuzaliwa baada ya kufikisha umri wa mika 116.
Misao ambaye anaishi chini ya uangalizi na matunzo huko Osaka, Japan alitangazwa rasmi kuwa mwanamke mwenye umri mkubwa zaidi duniani baada ya aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo kufariki.
Ingawa umri wake ni mkubwa sana, anaonekana bado ana afya nzuri na aliweza kuipuliza mishumaa yake kama mtu mwingine.

Lupita Nyong'o na Rihanna 'wapoz' pamoja, waing'arisha fashion Show jijini Paris.

$
0
0
Mshindi wa tuzo ya Oscar, Lupita Nyong’o, Jana (March 5) alihudhuria kwenye maonesho ya
mitindo ya wiki yaliyofanyika Paris inayojulikana kama ‘Miu Miu Fashion Show’, ambapo mastaa wengi walihudhuria ikiwa ni pamoja na Rihanna.
 Rihanna alikutana na Lupita Nyong’o ambapo walikaa pamoja na kupiga picha kadhaa ambazo zilipostiwa na Lupita Nyong’o.  
Kwa mujibu wa ripoti, wawili hao ndio waling’ara zaidi kimavazi katika show hiyo, huku Lupita akionekana kuwa mchangamfu na kuzitumia dakika 40 za mwanzo zilizoongezwa kwa ajili ya kumsubiri Rihanna kujitambulisha vizuri kwa wageni wengine waliokuwa wamekaa nae kwenye viti vya mbele.
Baada ya picha hiyo, wengi walianza kutoa maoni yao kwenye mitandao wakidai wanatamani kumuona Lupita Nyong’o kwenye video moja ya wimbo wa Rihanna.

Rick Ross kutolipiza chochote baada ya 50 Cent kumdhihaki kwa 'ushoga'

$
0
0
Lakini kwa mujibu wa chanzo cha mtandao wa TMZ, rapper huyo ambaye jina lake halisi ni William Leonard Robert II, hataupoteza muda wake kumjibu rapper huyo na kueleza sababu kuwa anamuona 50 Cent hana umuhimu kwake.
Imeelezwa kuwa Rick Ross amepanga kuiacha hiyo issue ipite kimya kimya na yeye aendelee kujikita katika masuala muhimu ya kutengeneza ngoma kali.
Jumapili iliyopita, 50 Cent alipost kwenye Instagram picha inayomuonesha Rick Ross akimsogelea P.Diddy kama vile wanataka ku-kiss na akaandika kwa ufupi, “something ain’t right’.
Viewing all 2632 articles
Browse latest View live