
“ Wewe sio mwanamke niliyekuwa nakufikiria.. samahani, ila ninakuacha” Bwana harusi alijikuta akisema maneno hayo siku ya ndoa baada ya kukutana uso kwa uso na Bibi harusi siku ya ndoa yao huko Saudi Arabia.
Wageni waalikwa walishtuka, Bibi harusi akapoteza fahamu huku ndugu na jamaa wakimsihi jamaa akubali ndoa hiyo iendelee.
Utamaduni wa Nchi za Mashariki ya kati, Magharibi mwa Madinah wapenzi huweza kuoana hata bila kufahamiana, ambapo mbali na kali hiyo kuna mwanaume mwingine anafanya utaratibu wa kudai talaka kutokana na mke wake kutomjibu message anazomtumia kwenye Whatsapp.